Friday, July 17, 2015

BANZA STONE AFARIKI DUNIA MCHANA HUU




Mwanamuziki wa muziki wa dansi aliyepata kushika chati za juu katika utunzi na uimbaji katika bendi mbalimbali nchini za muziki wa Dansi ,  Ramadhani Masanja 'Banza Stone' amefariki dunia hii leo mchana nyumbani kwao Sinza Kijiweni Dar es Salaam.
Nyota huyo wa zamani wa bendi hiyo ya Twanga Pepeta na Tot alikuwa akiumwa kwa muda mrefu.
Mmiliki wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka amethibitisha kifo cha Banza Stone.
"Ni kweli amefariki leo mchana saa saba, baada ya kutoka msikitini ndiyo tumepata taarifa hizo za msiba," alisema Asha Baraka.
Mara kadhaa, Banza amekuwa akizushiwa kifo kupitia mitandao na vyombo mbalimbali vya habari.

0 comments:

Post a Comment