Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa
361 Digrees, Hamis Omary akizungumza katika mkutano na waandishi wa
habari Dar es Salaam leo kuhusu maandalizi ya maonesho ya Harusi Trade Fair 2014 yatakayofanyika Aprili 11 na 12, 2014 katika viwanja vya Parthenon Hall (Greek Club)
Ofisa Habari wa 361 Digrees, Abisai Mbwana (kushoto), akitoa neno fupi la ukaribisho kwa wanahabari.
Meneja wa Maendeleo
ya Biashara wa 361 Digrees, Hamis Omary akizungumza katika mkutano na
waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu maandalizi ya maonesho ya
Harusi Trade Fair 2014 yatakayofanyika Aprili 11 na 12, 2014 katika
viwanja vya Parthenon Hall (Greek Club)
Na Dotto Mwaibale
WATU wanaotarajia kufunga harusi
wametakiwa kujipanga kwa kufanya maandalizi mapema kwa kuwa siku hiyo ni
muhimu katika maisha yao na haistahili kubezwa.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar
es Salaam na Meneja Biashara na Maendeleo wa Kampuni ya 361, Hamis Omary
inayojihusisha na maonesho ya harusi nchini.
Alisema watu hudhani harusi ni jambo
la kawaida na wakati mwingine kupuuziwa lakini ni jambo kubwa kiimani na
la kihistoria katika maisha linalopaswa kuungwa mkono na jamii.
Omary alisema maonesho ya harusi
ambayo hufanywa na kampuni hiyo yametimiza mwaka wa tano ambapo mwaka
huu yatafanyika kesho na kesho kutwa katika viwanja vya Parthenon.
Asema maonesho ya mwaka huu
yameandaliwa na wabunifu mbalimbali na kwamba ni maonesho ya wazi hivyo
kila mtu anakaribishwa kuhudhuria kujifunza mambo yanayohusu harusi na
namna ya kuifanya siku ya harusi kuwa ya kuvutia.







0 comments:
Post a Comment