Friday, November 29, 2013

KINANA, NAPE WASISITIZA MAWAZIRI MIZIGO KUSHITAKIWA KAMATI KUU YA CCM

 Wananchi wa Kijiji cha Ntunduru, Kata ya Isansa, wilayani Mbozi, Mbeya, wakisikiliza hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo leo, huku wakiwa wamejikinga mvua kwa kutumia viti.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia), Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro (wa pili kulia), Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mbeya, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi (wa tatu kulia) pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakipanda miti katika Zahanati mpya ya Ntunduru, Kata ya Isensa, wilayani Mbozi, wakiwa katika ziara ya
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro na Kinana wakitoka kwenye nyumba ya Balozi wa Shina la CCM, katika Kijiji cha Ntunduru, Mbozi, ambapo alizungumza na wanachama wa shina hilo.
Kama kawaida yake, Kinana akishiriki katika ujenzi wa jengo la Zahanati ya Ntunduru
Kinana akiangalia moja ya vikundi vilivyokuwa vikitumbuiza alipofika katika Kijiji cha Ntunduru.
Kinana akimwangalia msanii wa sarakasi Huruma William anayefanya maajabu ya kutembea kwenye kamba
Msanii wa muziki wa kizazi kipya wa kikundi cha Pa si Ilembo, Michael Ilembo, aghani wimbo wa CCM alipotumbuiza katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ntunduru, wilayani Mbozi.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ntunduru.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi, akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ntunduru, katika Kata ya Isansa, Mbozi.
Kinana akivishwa mgolole na kupewa silaha za asili ikiwa ni ishara ya kumsimika kuwa mmoja wa viongozi wa jadi wa kabila la Wanyiha, wilayani Mbozi.
Kinana akiwasalimia wananchi alipokuwa akiingia kwenye mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Stendi ya Malori, mjini Mbozi, ambapo alihutubia na kusisitiza kuwa mawaziri mizigo hawatawaonea haya kuwasema kwani hawawatendei haki wananchi na CCM pia.
Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro, akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Mbozo, ambapo alisisitiza suala la elimu kwa watoto pamoja na kupiga vita unyanyasaji kwa wanawake.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye,akihutubia katika mkutano wa hadhara mjini Mbozi, na kumtaka Waziri wa Kilimo, Ushirika na Chakula kuacha tabia yake ya kila mara kuongea kwenye magazeti kwamba Nape atumiea busara anapozungumzia matatizo ya utendaji wake kuhusu matatizo ya wakulima nchini. Nape alisisitiza kuwa suala ya kumpeleka Chiza kwenye kikao cha Kamati Kuu kujieleza halikwepeki. PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA


KATIBU wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amemtaka Waziri wa kilimo, Chakula na Ushirika kuacha kumshambulia kwenye vyombo vya habari na badala yake atumie muda huu kuandaa majibu ya kuwasilisha mbele ya Kamati Kuu kutokana na hoja zilizoibuliwa na wakulima nchini.
Akihutubia mamia ya wananchi wa mji wa Mbozi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana wilayani hapa Nape, alionyesha kukerwa na tabia ya Waziri Chiza kumshambulia kwenye vyombo vya habari  kwa kwa maneno ya kejeli.
“Ndugu Katibu Mkuu tumezunguka wilaya nyingi nchini hakuna mahali ambako hakuna malalamiko ya wakulima ambao ni asilimia 80 ya watanzania wote. Kutokana na hali hii sasa tunamtaka waziri Chiza aje mbele ya CC mwezi ujao na kueleza anatatuaje changamoto hizi.
“Yeye amekazana kila kukicha kunishambulia kwenye magazeti. Nataka kumpa ushauri wa bure mheshimiwa sana waziri, anachofanya hanishambulii mimi anawashambulia wakulima kwa sababu siongei masuala yangu binafsi ila niongealea malalamiko ya wakulima,” alisema Nape
Alisema amemvumilia kwa muda mrefu ila kwa sasa amechoka, ambapo  kila kukicha Waziri huyo amekuwa akitumia maneno ya kejeli na vijembe huku akimtataka kujifunza  busara ya Naibu wake Adam Malima.
“Malima aliposikia wito wetu akasema yuko tayari kuja kujieleza kwenye Kamati Kuu kwa kuwa chama ndiyo mwajiri wake hivyo atazingatia maamuzi ya chama, yeye waziri kila kukicha Nape Nape Nape, kunishambulia hakuondoi kero za wakulima.
"Nimesikia leo anasema sina busara!! busara ipi anayohoji? Mie ninayewatetea wakulima wanaolalamika kulazimishwa kutumia mbolea ya Minjingu inayounguza mazao yao na yeye anayeleta mbolea hiyo na kulazimisha wakulima watumie nani anatumia busara hapa.
“ Yeye anayepuuza malalamiko ya wakulima kuumizwa na baadhi ya maafisa ushirika na mimi ninayetaka hatua zichukuliwe dhidi ya maofisa wake nani anatumia busara??,” alisema na kuhoji.
Mwisho

0 comments:

Post a Comment