Friday, May 18, 2012

JAGUAR, PREZZO BEEF NJE NJE



Jaguar na Prezzo
Katika hali inayoashiria kuwa beef kati ya Msanii Prezzo na Jaguar wote wa nchini Kenya, Jaguar ameibuka na kumponda Prezzo kuwa hana lolote katika muziki.
Jaguar ambaye jina lake halisi ni Charles Njagua amesema kuwa Prezzo ni mwanamitimindo na sio mwanamuziki na hivyo hawezi akashindana na yeye.
 “Prezzo sio mwanamuziki me namuona kama  model kwakuwa ameshinda category ya Best Dressed katika tuzo za Chaguo La Teeniez  mara moja, basi hawezi shindana na mimi kivyovyote” alisema.


Jaguar alisema kuwa hata linapokuja suala la fedha hawezi akashindana nae kwa kuwa yeye ana mafanikio makubwa kuliko Prezzo,  alisema kwa sasa anamiliki gereji ya kisasa inayoitwa Jagz Auto iliyopo mjini Nairobi, kampuni ya taxi iitwayo Jagz cabs na kampuni ya ulinzi iitwayo Jagz Security.
“Prezzo hawezi kuongea kuhusu hela kwasababu ntamuumbua katika kitengo hicho hasa pale tutakapoamua kutangaza mali zetu" aliongeza.

0 comments:

Post a Comment