Saturday, April 7, 2012

REST IN PEACE KANUMBA THE GREAT


Usiku wa kuamkia leo Msanii wa Bongo Movie Steven Kanumba amefariki dunia baada ya kuangukia kisogo kwa kile kinachodaiwa kusukumwa na mpenzi wake Lulu. Kwa mujibu wa mdogo wa msanii huyo alisema awali kulikuwa kuna mzozo baina ya kanumba na Lulu ambapo waliamua kuingia ndani ili waweze kumaliza mzozo huo lakini baada ya muda Lulu alitoka na kumuita mdogo wa Kanumba aje amuangalie kaka yake ameanguka baada ya kuingia ndani na kumkuta kaka yake ameanguka ilibidi aende akamuite daktari na aliporudi alikuta Lulu ameondoka.
Chanzo cha mzozo huo inadaiwa kuwa ni Lulu kuongea na mwanaume mwingine kwenye simu hali iliyopelekea kuzuka kwa mzozo huo.
Inasemekana Lulu tayari ameshakamatwa na anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Osterbay.
               REST IN PEACE OUR KAKA MKUBWA              STEVEN KANUMBA ‘THE GREAT’

0 comments:

Post a Comment